Header Ads

TUMIA MIFANO HII KUJIULIZA KAMA UNAELEWA UMUHIMU WA NAFASI ULIYO NAYO KATIKA KUMTUMIKIA MUNGU

Mfano wa OBADIA
4 kwa kuwa ikawa, Yezebeli alipowaua manabii wa Bwana, Obadia akatwaa manabii mia, akawaficha hamsini hamsini katika pango, akawalisha chakula na kuwapa maji).
12 Na itakuwa, mara mimi nikiondoka kwako, roho ya Bwana atakuchukua uende nisikojua; nami nitakapokwenda kumwambia Ahabu, naye asipokuona, ataniua, lakini mimi mtumishi wako namcha Bwana tangu ujana wangu.
15 Eliya akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo ambaye ninasimama mbele zake, hakika nitajionyesha kwake leo.
1 Waf 18
Obadia aliishi kwenye nyumba ya Yezebeli aliyekua amejaa uovu sana lakini alikua MCHA MUNGU. Huu uchaji ndio ulimsukuma kuwaficha manabii wa Mungu saa Yezebeli anataka kuwaua. Mungu alimpa ile nafasi ili aweze kujua siri zinazoendelea ikulu juu ya watu wa Mungu. Kuna nafasi Mungu anakupa ili ukusanye data za kusaidia watumishi wake. Usije ukafikiri Mungu akikuweka kuwa mkandalasi wa wilaya hakuna analotaka ufanye kwa ajili yake. Nafasi yako ni ya muhimu kuliko unavyo dhani katika kulitunza shauri la Mungu.
Ukiacha kuitumikia iyo nafasi Mungu amekupa uwe na uhakika anao uwezo wa kukuondoa. Kumbuka jinsi Mordekai alivyo mwambia Esta juu ya nafasi ya umalikia kwenye nchio ya ugeni. Kama Esta angekaa kimya Mungu angewainulia msaada toka mahali pengine kuwasaidia wayahudi.
Sasa huenda nawe ni kama Esta, pamoja na kuwa na nafasi mahali fulani lakini hujui maana ya iyo nafasi kwa jicho alilonalo Mungu. Kama Mordekai alimkumbusha Esta name nakukumbusha kupitia somo ili, ukikaa kimya kwenye iyo nafasi Mungu atatumia namna nyingine na kuachana na wewe.
Swali nataka ujiulize
·         Kwa nini Obadia katika kujitetea ili Elisha aende kujionyesha kwa Ahabu ilibidi neno “namcha Mungu tangu ujana wangu liandikwe”? Kulikua na sababu gani ambalo uchaji ilikua lazima kuandikwa? Nini Mungu alitaka tujue kuhusiana na uchaji?

7 Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Mith 1
6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.
Hosea 4
Nataka uone hapo, sababu ya watu wa Mungu kuangamia inaonekana ni kukosa maarifa. Mtu mchaji ana haya maarifa ambayo kimsingi pia yatamsaidia asiangamizwe. Ukisoma Hosea ni kwamba asiye na maarifa yuko kwenye hatari ya kuangamizwa.
Obadia kutokana na uchaji wake alikua na maarifa, na alijua kabisa kama akikubali kazi aliyopewa na Eliya ya kwenda kumsimulia Ahabu kwamba walikutana na Ahabu asimuone ndo ingekua mwisho wake na angeangamizwa. Sasa maarifa yalimsaidia kupangua hoja ya Eliya na matokeo yake wakaenda wote kwa Ahabu.
Nataka uone ukiwa unamtumikia Mungu unahitaji maarifa sio kawaida. Kuna watu utakutana nao ambao utahitaji maarifa kupangua hoja zao vinginevyo watakutengenezea mitego uangamizwe. Na wanaweza kuwa ni watu wa Mungu kama ilivyo kwa Eliya.
Sasa agano jipya ngazi moja ya uchaji inaongezeka. Utakumbuka Matendo 10 kuhusu habari ya Konelio. Huyu bwana alikua mchaji sana lakini hakuwa ameokoka. Uchaji utaji utakusaidia utakua na mahusiano mazuri na Mungu lakini roho yako haiwezi kwenda Mbinguni bila kumpokea Yesu. Konelio alihitaji atoe maisha yake kwa Yesu ili uchaji wake uwe na maana zaidi. Kufuatana na biblia Yesu ni NJIA, KWELI na Uzima mtu haendi kwa Baba ila kwa njia ya Yeye. Maana yake ni kwamba kama hujampokea Yesu uchaji wako utakusaidia tu hapa duniani ila huna makao kwa Baba mbinguni.

Mfano wa NAAMAN
1 Basi Naamani, jemadari wa jeshi la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake Bwana alikuwa amewapa Washami kushinda; tena alikuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma
2 Na Washami walikuwa wametoka vikosi, wakachukua mfungwa mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani.

 3 Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake.
15 Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako.
2 Waf 5
Uwezo na heshima aliyokuwa nayo Naamani ilitoka kwa Bwana. Lakini pamoja na kumpa iyo heshima lakini alimuacha na ukoma kwenye mwili wake. Usije fikiri Mungu hayuko kwa sababu ya tatizo unaloliona kwako lijaondolewa, Mungu anabaki kuwa Mungu hata kama unafikiri hajakuondolea ilo tatizo lako.
Biblia haielezi wasifu wa huyu dada aliyechukuliwa kama mateka toka Israeli ila tendo alilolifanya linatosha kuonyesha huyu dada alitambua uwezo uliopo kwa Mungu vizuri ndio sababu alitoa ushauri wa aina ile. Sio rahisi kwa house girl kutoa ushauri wa aina ile kwa bosi wake kama hana uhakika nao. Nataka uone pamoja na nafasi ndogo sana aliyokua nayo yule binti lakini hakukaa kimya na kuacha kuelezea habari za Mungu wake. Nakumbusha tena, kwa nafsi yeyote uliyo nayo unaweza kulitumikia kusudi la Mungu, kikubwa ni kwamba hapo ulipo usiache uchaji. Mazingira uliyo nayo yasiondoe uchaji wako.
Jaribu kufikiri huyu mdada angejinyamazia nini kingetokea? Ni kweli Mungu aliacha ukoma kwenye mwili wa Naaman pamoja na kumpa heshima sana lakini ule ukoma Mungu aliuacha kama mtaji kwa ajili ya mtu mwingine kutambulika. Fikiri kama dada alsingetoa ushauri wa jinsi ile kama angeandikwa kwenye biblia.
Nafasi uliyo nayo Mungu anangoja uitumie kulitenda kusudi lake akutambulishe mbele za wengine, upige hatua moja zaidi. Ile nafasi dada alivyoitumia ndiyo iliyo mtambulisha Mungu wa Israel kwa Naaman. Pamoja na kwamba ni Mungu alimpa ile heshima ila Naamani hakuwa anamjua Mungu wa Israeli. Unaweza kukaa kimya ukifikiri ulio nao wanamjua Mungu kumbe hawamjui na Mungu amekuweka hapo ili umtambulishe kwao.

Mfano wa VIJANA WASOMI KINA DANIEL
3 Mfalme akamwambia Ashpenazi, mkuu wa matowashi wake, awalete baadhi ya wana wa Israeli, wa uzao wa kifalme, na wa uzao wa kiungwana;
4 vijana wasio na mawaa, wazuri wa uso, wajuzi wa hekima, werevu kwa sababu ya maarifa yao, wenye kufahamu elimu, watakaoweza kusimama katika jumba la mfalme; tena alimwambia awafundishe elimu ya Wakaldayo, na lugha yao.
Dan 1
“Awalete baadhi” maana yake walikua wengi ila hakuwataka wote, kwa ivyo hao baadhi walio patikana kwao ilikua ni zaidi ya bahati.
Lakini nataka uone kosa kubwa ambalo Danieli hakulifanya kama ambavyo watu wengine wakipewa nafasi Fulani huwa wanafanya ilo kosa. Ukisoma vizuri utaona udahili wa hao vijana pia ulikua na lengo la kudahiliwa. Lengo la wao kudahiliwa ni ili wasimamie kusudi la mfalme ila sio la Mungu. Ni rahisi sana mtu ukahajiliwa mahali kisha ukasahau kwamba pamoja na kuwepo lengo la ofisi lakini lengo kubwa la Mungu kukuweka hapo na sio kumweka mwingine ni ili wewe utunze kusudi lake hapo. Fikiri kwamba kuna watu wengi mtaani wenye sifa kama za kwako lakini hawako kwenye iyo ofisi na ujiulize ili swali kwa nini wewe?. Usije hata siku moja kusingizia ofisi yako kuwa ndio imefanya ukose nafasi ya kumtumikia Mungu.

Ni sawa kabisa unaweza kufikiri ukiwa shule lengo lako ni kusoma tu, lakini fikiri mara mbili kwamba ni kweli hao ulio waacha mtaani na hawakupata nafasi ya kusoma kweli Mungu hana mpango nao?. Utakuja ugundue huko kwenye nafasi uliyo nayo only kwa ajili ya kusudi la Mungu Fulani ambalo huwezi kulitekeleza kama ungekua nje na hapo shuleni.

Mambo ambayo Danieli alikuaja kuyafanya kwenye sura ya pili na akuendelea ilimuhitaji kwanza kuipata ile nafasi ya kudahiliwa kisha kumtumikia Mungu hata kwenye ile nafasi.




 
Theme images by centauria. Powered by Blogger.