BWANA MUNGU WAKO ANATAKA NINI KWAKO KABLA YA KUMTUMIKIA?
“Na
sasa, Israel BWANA MUNGU wako anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako,
na kwenda katika njia zake zote na kumpenda na kumtumikia BWANA MUNGU wako kwa
moyo wako wote na kwa roho yako yote.” Kumb 10:12
Sio watu wengi sana wanafuatilia hili swali kabla ya
kuanza kumtumikia Mungu katika maisha yao kwa nafasi Mungu alizowapa. Mambo
anayotaka uyafatilie ni;-
1.
Umche
2.
Kwenda
katika njia zake zote
3.
Kumpenda
Baada ya mambo haya matatu ndipo Mungu anaachilia
nafasi ndani ya mtu kwa ajiri ya yeye kuitwa mtumishi wake.

Kumb 10:20
“Mche
BWANA MUNGU wako, umtumikie yeye, ambatana naye na kuapa kwa jina lake.”
Isikusumbue kwa sababu unatumika kanisani ukajipa
uhakika unamtumikia Mungu, ni vizuri kufuatilia hatua alizioweka nyuma kabla ya
utumishi. Wako watu wanatumika vizuri kanisani lakini si watumishi wa Mungu.
Mfano
: Kwa Yoshua, Yosh 1:1
“Ikawa
baada ya kufa kwake Musa, mtumishi wa BWANA, BWANA akamwambia Yoshua mwana wa
Nuni, mtumishi wa Musa , akasema……..”
Ndugu Yoshua yote aliyokuwa akifanya hapo nyuma biblia
inatupa kujua alifanyika mtumishi nyuma ya Musa. Nafasi ya utumishi ilikuwa
sasa halisi kama mtumishi wa Mungu kwa sababu huyu ndugu alifatilia yale mambo
ya msingi matatu.
Ukiendelea kusoma mistari ya hapo utaelewa na mimi ya
kwamba hapo kabla kama alikuwa anamsikia Mungu si katika kiwango kile alichokua
nacho Musa, ndio sababu Mungu anampa uhakika ya kwamba nitakuwa na wewe katika
kiwango kile kile nilichokuwa na Musa bila hata kukupungukia.
Yosh 1:5
“…….kama
niliyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakupungukia
wala kukuacha…..”
Nisingekuuliza swali hili nililokuuliza ulipaswa
kujiuliza swali la hivi “ Bwana Mungu
anataka nini kwako?” hii ni kutokana na kitabu tulichokisoma cha kumbukumbu
la Torati. Ukijiuliza hili swala la Bwana Mungu anataka nini kwako unatakiwa
kujua mambo yafuatayo:-
1.
Umche
yeye
2.
Kwenda
katika njia zake zote
3.
Kumpenda
4.
Kumtumikia
kwa moyo wako wote na roho yako yote
5.
Kuzishika
amri zake alizokuamuru
Baada ya kuangalia haya mambo matatu Mungu
anakuhakikishia ya kwamba mbingu ni mali zake ,mbingu za mbingu, na nchi na
vitu vyote vilivyomo. Maana yake ni kwamba anakupa uhakika wa kutokuwa masikini
na kuangaika na maisha kwa namna yoyote ile baada ya kuyaangalia hayo mambo
matano.
Sasa mimi nimeweka haya mambo matatu kabla ya utumishi
kwa sababu nasikia msukumo wa kukupatia maelekezo ya kutosha kukusaidia katika
utumishi ulio mbele yako. maana biblia inasema si wote waitao Bwana Bwana
watauona ufalme wake.
Math 7:17-23
“Si
kila mtu aniambiaye ,Bwana Bwana atakaye ingia katika ufalme wa mbinguni; bali
ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku
ile Bwana………”
Hapa ndugu Matayo anajaribu kuzungumza na watumishi
ambao wajazingatia yale mambo matatu nimekueleza hapo juu. Na ninapokufundisha
haya ninataka utoke katika kundi la watumishi watakao lalamika huko mbinguni.
Lakini si hayo mambo matano tu Mungu anahitaji toka
kwako ni zaidi ya hayo, kwa mfano unapoonganisha kitabu cha kumbukumbu la
torati na kitabu cha Mika utagundua Mungu anataka mambo takribani nane toka
kwako.
Mika 6:8
“ Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema, BWANA anataka
nini kwako ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na
Mungu wako.”
Hivyo unapata kujua mambo yafuatayo ambayo Mungu
anataka kwako;
1.
Umche
yeye
2.
Kwenda
katika njia zake zote
3.
Kumpenda
4.
Kumtumikia
kwa moyo wako wote na roho yako yote
5.
Kuzishika
amri zake alizokuamuru
6.
Kutenda
haki
7.
Kupenda
rehema
8.
Kwenda
kwa unyenyekevu na Mungu
KWENDA
KATIKA NJIA ZAKE ZOTE
Unapoanza kumtumikia Mungu katika nafasi yoyote ile
tunategemea kuona unafanikiwa na unasitawi sana. Chukua somo ili kama mtaji wa
kujitafakari…..ASANTE