Header Ads

UNAUTAZAMAJE UZINZI KATIKA MAISHA YAKO NA KRISTO


Image result for joseph son of Jacob rum from Potiphar wife pictures

‘lakini mimi nawambia, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini moyoni mwake.’  Math 5:28

‘Ikimbieni zinaa, Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.’  1Kor 6:18

Uzinzi kama uzinzi una matokeo katika mwili na roho ya mwanadamu. Lakini waliowengi wamekuwa wakifuatilia matokeo ya uzinzi katika miili yao na mara chache katika roho zao.
Uzinzi una matokeo mengi kati ya hayo ni pamoja na
·        Kuingiza miungu ya mtu unayezini naye
·        Kumwagiwa uzinzi na unayezini naye
·        Kupata ukimwi na magonjwa mengine
·        Kupata mimba usiyo tarajia
Kuingiza miungu ya kigeni kwa njia ya uzinzi
Unapofanya uzinzi na mtu jua kwamba pia unafanya ilo tendo na miungu yake hivyo unaikaribisha kwako.
‘…..watu wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao……’  Kut 34:15, 12
Kuna athari za kuingiza miungu ya kigeni katika maisha yako mkristo. Kuingiza miungu ya kigeni kupitia tendo la ndoa maana yake ni kufanya agano na hiyo miungu. Na kinachotokea unapofanya agano na miungu migeni inakaa katikati yako.

Kilichomtokea Selemani mfalme
Selemani alikaribisha miungu ya kigeni kwa njia ya tendo la ndoa

JINSI GANI UNAWEZA KUEPUKA UZINZI
Biblia imetoa ushauri mmoja mkubwa sana wa moja kwa moja juu ya nini cha kufanya ili kuepuka uzinzi.
Kabla sijakwambia jinsi ya kuepuka nikukumbushe jambo hili. Uzinzi ni uzinzi pamoja na makundi yake yote isipokua matokeo ya uzinzi ni tofauti katika muonekano wake. Kuna watu ambao wanazini kwa mawazo lakini si kwa tendo kama wanavyosemwa katika Mathayo
‘lakini mimi nawambia, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini moyoni mwake.’  Math 5:28
Na kuna watu ambao wanazini kwa tendo na kwa mawazo nao ni wazinizi.
Lakini ushauri wa moja kwa moja wa kibiblia kwa makundi yote haya ni kuukimbia.
‘Ikimbieni zinaa, Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.’  1 Kor 6:18
Unaukimbiaje uzinzi kwa njia ya mawazo?
Uzinzi wa kimawazo unakimbiwa kwa kuepukana na mazingira shawishi. Kwa mfano kama hutaki uzinzi wa kimawazo usiangalie picha za wadada wakiwa watupu, picha za ngono n.k au usikae mahali wanakozungumza stori za kuzini.
Ninakwambia hivi kwa sababu hiki ndicho kitu kilichomsaidia Yusufu hakutaka stori na yule mke wa mfalme.
‘Akawa akazidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye.’  Mwa 39:10
Kwa sababu uzinzi wa mawazo unafanyikia moyoni kwanza kabla ya mwilini ni vizuri kuujaza moyo neno la Mungu kiasi ambacho hakuta kuwa na nafasi ya kitu kingine. Maana biblia inatuambia kama moyoni kumejaa neno na kiukweli unalifuata huwezi kutenda dhambi kabisa.
‘moyoni mwangu nimeliweka neno lako nisije Bwana nikakutenda dhambi mimi.’

Uzinzi wa mwili unakimbia vipi?
Tujifunze kwa Yusufu tena
‘huyu mwanamke akamshika nguo zake,akisema , Lala name. Yusufu akaiachia nguo yake mikononi mwake akakimbia, akatoka nje’  Mwa 39:12

Nataka uyaone haya maneno mawili
·        Akamshika nguo zake
·        Akatoka nje
Wako wadada/wakaka hadi wanavuliwa nguo bado wanashangaa tu wakati Yusufu aliposhikwa tu akili ilichange. Sasa wewe unashikwa nguo still utoki nje unategemea kitu gani mtumishi.
Haiwezekani kwamba hutaki uzinzi na bado unakaa chumbani na mwanaume/mwanamke unayemtamani.

Mwisho
Theme images by centauria. Powered by Blogger.