Header Ads

JE KUFANIKIWA KWAKO KUNATEGEMEA NINI?


Mtu yeyote aliyeokoka anao uwezo wa kuishi na kuwa na uhakika ama atakuja kufanikiwa katika maisha ama hatofanikiwa.Nina maana kwamba mtu yeyote aliyeokoka anaweza kujua wapi anaelekea kabla ya kupafikia. Kwa sababu ifuatayo;
·         Mtu aliyeokoka ana uwezo wa kumuuliza Mungu kwa habari ya mambo yatakayokuja.
“BWANA ,Mtakatifu wa Israeli na Muumba wake asema hivi, Niulize habari za mambo yatakayokuja;mambo ya wana wangu na habari ya kazi ya mikono yangu,haya!Niagizeni.”  Isa 45:11
Kama Mungu anatupa mwaliko wa kwenda na kumuuliza habari za mambo yatakayokuja sasa ni kwa nini mtu aliyeokoka ashindwe kuyajua maisha yake yajayo?.Tatizo la watu wengi waliookoka ni wazuri katika kuombea mapepo ama kuziombea huduma mbalimbali ila sio kuyaombea maisha yao.
Na ili swala la kumuuliza Mungu habari zitakazokuja ni la mtu binafsi sio la kikundi.
·         Mungu mwenyewe anaweza kujifunua kwako na kukupasha habari zako zijazo.
Sote tunakumbuka haikumuhitaji Yusufu kufunga na kuomba ili Mungu amwambie habari za maisha yake yajayo isipokuwa Mungu mwenyewe alijifunua kwa njia ya ndoto.    Mwanzo 37:3-6
Kuna watu leo tunao ndani ya kanisa ambao Mungu alikwisha sema nao mahali watakuwepo kwa njia yoyote ile aliyosema nao lakini bado wanaishi kwa kubahatisha.Tatizo la watu wengi nimegundua sio kusemeshwa isipokuwa kuelewa kile walichosemeshwa.
Watu wengine wengi wamekwama katika maisha kwa kufikiri kufanikiwa kwao katika maisha kunamtegemea mtu.Biblia inatupa kuona ya kwamba mtu hafanikiwi kwa sababu kuna mtu aliomtoa isipokuwa tunachokiona ni kwamba mtu anafanikiwa kwa kuletewa msaada na Mungu.

Kufanikiwa kwako hakutegemei wala hakuzuiwi na sababu yoyote ile uliyo nayo. Kwa mifano;
1.      Sababu za kimadhingira
Kuna kundi kubwa sana la walokole wamezidi kubaki katika hali zao kutokana na kuamini kwamba maeneo waliyopo hawawezi kufanikiwa.
Unapaswa kujua kwamba hakimpi Mungu shida wewe kuzaliwa familia uliyozaliwa.Kuna watu wakiangalia historia za maisha yao kiuchumi hawafikiri kabisa ya kwamba yuko Mungu ambaye anaweza kupita katikati na kubadilisha hali yao ya maisha.Umewai kufikiri kama Daudi kwa madhingira ya kifamilia aliyokuwa akiishi angeweza kutoka kimaisha hadi kuwa mfalme?  1Sam 16-17
Hakimpi Mungu shida ya kwamba umesoma vidato vingapi ndipo hakufanikishe katika maisha.Watu wengine wengi wamekwama tu eti kwa sababu wanajiona wajasoma kabisa.Mimi sijui ni nani aliyekwambia kama hujasoma huwezi kufanikiwa.Ingekuwa kusoma ni kufanikiwa basi kila aliyesoma ungemuona akiishi maisha mazuri.Sasa kwa sababu watu wengine hawajasoma basi wamejitengenezea mipaka sana katika maisha yao.,kwa mfano utakuta mtu ana karama ya kuhubiri lakini hajawai hata siku moja kwenda kuwahubiri wasomi akifikiri sio saizi yake.Ivi umewai kuona ni wapi katika biblia Yesu anaenda shule?lakini bado huyu huyu Yesu tunaona anawashinda wanasheria wa kiyahudi.Sasa sina maana ya kwamba kusoma ni kubaya hapana.
Ile kwamba kabla ya kuokoka umekuwa mdhambi sana si sababu ya Mungu kutokufanikisha leo ulipoamua kumuishi naye.Watu wengi wamewai kusikia ndani yao hali ya kutaka kumtumikia Mungu na wanaposikia hivyo mara moja wanaona mafanikio mbele yao lakini kiko kitu kinawahukumu ya kwamba hawawezi.Ingekuwa ni hivyo basi Paulo asingefika popote kitumishi kwa sababu historia yake ya kimadhingira ilikuwa ni mbaya sana  Mdo 6-.Akina Rahabu basi wasingefika popote kama ni vivyo maana Rahabu historia yake ya kimaisha sote tunaijua Yoshua 2.Unajua nimesema hii kitu kwa sababu walokole wengi ambao neema ya Mungu ilifunuliwa kwao kabla na wakaishi maisha ya kiroho mapema wanawahukumu wenzao eti.Kuna wadada wanafikiri kwa sababu hawakuwai kufanya uzinzi basi wamestahili sana kuliko wenzao.Sasa unielewe vizuri sina maana uzinzi ni mzuri.

2.      Sababu za kiumri
Watu wengine wamejitazama idadi ya miaka waliyo nayo wakafikiri ni kigezo cha wao kutokufanikiwa.Wengine umri kwa sababu ni mdogo wamefikili hawawezi kufanya vitu wakafanikiwa.Na sijui nani kawambia hiyo kitu.Na hata kanisa nalo limewakwamisha watu wengi sana wasipige hatua kwa sababu ya umri walio nao.Utakuta watoto wadogo katika kanisa wanawekwa nyuma nyuma kwa sababu wao ni wadogo.
Mifano;
·         Mfalme Uzia,1nyak 26:3
·         Mfalme Manase,1nyak 33:1
·         Mfalme Yosia,1nyak 34:1
Sasa kama Mungu aliwatumia akina Yosia mabwana wadogo kiasi hicho kwa nini wewe angoje uwe mkubwa ndipo akutumie?
Watu wengi hawafahamu hii kitu,Mungu akitaka kukutumia hakuhakikishi idadi ya umri wako isipokuwa kuna vitu ni vya muhimu ambavyo huwa anavihakikisha.Na akivikuta viko sawasawa ndipo anakuinua na kukutumia pasipo kuangalia kigezo chochote ulicho nacho.

Mfano wa Yeremia.
“Tena neno la Bwana likanijia kusema,Yeremia waona nini?nikasema naona ufito wa mlozi.Ndipo Bwana akaniambia umeona vema kwa maana naliangalia neno langu ili nilitimize.Neno la Bwana……………….”             Yer 1:11-12
Kabla ya kukuinua katika huduma na kukufanikisha haya ni baadhi ya mambo Mungu anayoyahakikisha;
      i.        Fikra yako
     ii.        Macho yako
    iii.        Kusikia kwako
Macho ya Yeremia
Hapo alichokuwa anakifanya Mungu ni kuyahakikisha macho ya Yeremia kama yanaona sawa sawa.

Fikra zako.
Kinachoweza kukuweka katika uongozi mkubwa katika ngazi ya siasa si umri wako ni fikra zako juu ya mambo.Watalaamu wanasema hivi “Leadership is not a position but an altitude.”maana yake ni kwamba unaweza ukawa na nafasi ya kuwa kiongozi lakini usiwe na fikra za uongozi.
Umri wako kuwa mkubwa pia sio sababu ya Mungu kutokukufanikisha.Watu wengi sana ambao umri umekwisha sogea wanakuaga na fikra potofu za kutokufanikiwa.
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi asema Bwana,ni mawazo ya amani wala si ya mabaya,kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”  Yer 29:11
Watu wengi wenye umri mkubwa wanaamini ya kwamba kama umri umepita wakashindwa kujikusanyia mali basi hiyo kitu hawawezi kuifanya katika umri wao.Hata mimi naungana nao kusema hivyo ya kwamba kama haukuwa tajiri wakati wa ujana wako huwezi kuwa tajiri siku zako za uzee kufuatana na mtazamo wa kisiasa.
Lakini mtazamo wa kibiblia uko tofauti kidogo,maana biblia inasema izo siku za mwisho kufanikiwa UTAPEWA na sio utatafuta.
Na kuna baadhi ya wazee wanajidanganya ya kwamba umri wa kuishi ni miaka sabini ila ukiwa na nguvu ni themanini.Zab 90:10……Mwa 6:3
SASA KUFANIKIWA KWAKO UWE NA UHAKIKA KUNATEGEMEA UNAVYOISHI NDANI YA KUSUDI AMBALO MUNGU AMEKUITIA KULIFANYA HAPA DUNIANI.
Ni vigumu sana kufuatana na ushauri wa kibiblia ukafanikiwa nje ya kusudi lako Mungu alilokuitia.Kwa hivyo ni lazima au ni muhimu kujua kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yako na ukajua thamani ya hiko kitu.
Kwa mfano;
Kama nyumbani kwako chini ya ardhi kuna madini halafu haukujua siku utakopoamua kupauza hapo utapauza kwa bei rahisi sana.Kama hautojua wewe ni nani hautojua thamani yako katika ulimwengu huu.
Ukiwa unafanya mambo ndani ya kusudi ambalo Mungu amekuitia kitu ambacho kinatokea ni kwamba mtu wako wa ndani anafanikiwa sana hadi kusababisha mtu wa nje kufanikiwa pia.
“Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yako na afya yako kama vile roho yako ifanikiwavyo.” 3Yoh 1:2
Mtu yeyote aliyefanikiwa hapa duniani alianzia rohoni kabla ya mwilini.Ndiyo maana biblia inatuambia cha kwanza kutafuta ni ufalme then vingine tutazidishiwa.
“Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hayo yote mtazidishiwa.”  Math 6:33
Hata wachawi wanaijua hii kanuni ya mafanikio ya kwamba mwilini kunafata baada ya rohoni kufanikiwa.
Kusudi kubwa ambalo Mungu amemwitia mwanadamu ni utumishi katika shamba lake.
1Kor 12:12-21+efe 4:15-16
Siku zote tunaishi ili tuujenge mwili wa Kristo na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetumika ndani ya kusudi la Mungu.Sasa katika kuujenga mwili wa Kristo wengine ni
·         wajenzi wa nje na
·         wengine ni wa ndani.
Ukijua wewe unakitu gani kiatamie katika maombi hadi kiwe dhairi mbele ya mioyo ya watu. Kwa mfano Yusufu alijua mapema sana tangu akiwa na umri wa miaka kumi na saba yeye ni nani katika taifa. Mwanzo 37:5-8
Lakini siku ilipofika hata wakuu wa nchi walijua ya kwamba hakuna mtu kama Yusufu kwa hivyo lazima wamtafute yeye.
Soma Mwa 40:1-15
Mambo tunayojifunza kutokea hapo.
a.    Usimuhudumie mtu kwa nguvu yote ya wito wako kwa sababu ya jinsi alivyo.
Tatizo la watu wengi wamegeuza utumishi wao kama source ya kupata pesa.Kwa mfano kilichomcost Yusufu alizani kwa kuwa amemuhudumia basi ataomtoa kimaisha yule mwokaji wa Mfalme ndio sababu alimwambia akitoka asimsahau.
b.    Usichague eneo la kumtumikia Mungu, ile tu Mungu kakuhakikishia nenda.
Yusufu angetazama kwa jinsi ya nje asingejisumbua kumtafsiria ndoto yule ndugu gerezani maana asingempa chochote even sadaka.Sasa kuna watu wengi wameshindwa kufanikiwa japo wako ndani ya kusudi la Mungu kwa sababu ya kuchagua chagua maeneo makubwa na yenye hadhi kwao.Utakutana na mtu kabisa ndani yake anaona kiu ya kufanya biashara fulani lakini anajiona kama atajishusha hadhi yake vile.
c.     Sababu za kimadhingira si kigezo cha wewe kutokufanikiwa.
Sio rahisi kukubaliana na hali aliyokuwa nayo Yusufu, maana ametoka gerezani hadi kuwa mkuu wanchi. Si rahisi kufikiri kama angeweza akatokea mtu na kumuokoa toka kule gerezani na kumpandisha.

MAMBO SABA YANAYOWEZA KUCHOCHEA MAFANIKIO YAKO.
Kitabu cha Yoshua 1:6-9 kinatuelekeza mambo hayo saba hapa chini;
      i.        Kuwa hodari/be strong
     ii.        Kuwa na moyo wa ushujaa/have courage
Having courage is about facing our fears and moving on in faith.
    iii.        Msikilize baba yako wa kiroho
    iv.        Lifanye neno la Mungu kama lako.
Ukiligeuza neno la Mungu kama ni lako itakupa urahisi wewe kulitafakari jinsi linavyohusika na maisha yako ya kila siku.Mungu alipomwambia Yoshua kitabu cha torati kisiondoke maana yake alitaka kiwe chake.

“Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako,bali yatafakari maneno yake usiku na mchana……..”
Tatizo linalowakumba wakristo wengi badala ya kutafari neno la Mungu wanatafakari ukubwa wa shida walizonazo.
     v.        Fata kile Mungu anakwambia kufanya.
    vi.        Anza kufanya jambo unalolisikia ndani yako./weka katika matendo ndoto yako.
Kama utakumbuka wakati ule wana wa Israeli wako katika bahari ya shamu maji hayakuwanyika hadi wameweka miguu yao ndani ya maji.Ni hatari sana ukaa na ndoto kichwani au moyoni isiyowekwa katika matendo.Wengi wameshindwa kuweka ndoto zao kwenye matendo kutokana na madhingira waliyo nayo.
  vii.        Usiogope
Theme images by centauria. Powered by Blogger.