KUMPENDA BWANA MUNGU WAKO
Marko 12:30-31
30 nawe
mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili
zako zote, na kwa nguvu zako zote.
31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende
jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.
Kumpenda
Bwana MUNGU kwa moyo ni pale mtu unapoamua
Kuokoka na kumkili kwamba ni mwokozi wa maisha yako. Kumpenda
kwa roho yako ni pale nafsi yako inapoamua kufanya kaz kwa kufuata maagizo ya
MUNGU. Nafsi
na moyo vyote uenenda sawa na MUNGU apendavyo.
Kumpenda
Bwana kwa Akili zako ni pale unapoamua kuamisha Upendo wako kutoka kweny nafsi
na mwili na kupeleka kwenye Akili na muda wote unawaza kumtumikia MUNGU na
kutumia nguvu kuyatenda mapenz ya MUNGU
NAMNA YA KUMPENDA
MUNGU WAKO
Kufuata amri na maagizo ya MUNGU
Amri
za MUNGU kwenye kutoka 20:1 zote zimemezwa na amri hii ya kumpenda Bwana MUNGU.
Kwani ukimpenda MUNGU huwezi kuiba, kuzini, kuua ,kuwa na miungu mwingine
Swali
Jiulize
leo unampenda MUNGU kweli au bado hujaamua? tafakari na uchukue hatua
Ameeen
na MUNGU akubariki