Header Ads

MUNGU AKIKUPA UWEZO KATIKA JAMBO FULANI HAINA MAANA HUMUHITAJI TENA


17 Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto.
Dan 1
Ni Mungu aliyewapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekina wakina Danieli na rafiki zake japo Danieli aliongezewa kitu cha ziada Zaidi ya rafiki zake. Danieli alipewa pia ufahamu katika maono yote (any kind of vision) na ndoto.

16 Basi Danieli akaingia, akamwomba mfalme ampe muda, kisha yeye atamwonyesha mfalme tafsiri ile.

17 Ndipo Danieli akaenda nyumbani kwake, akawapasha habari kina Hanania, na Mishaeli, na Azaria wenzake;

18 ili waombe rehema kwa Mungu wa mbinguni kwa habari ya siri hiyo, ili kwamba Danieli na wenzake wasiangamizwe pamoja na wenye hekima wa Babeli.

19 Ndipo Danieli alipofunuliwa siri hiyo katika njozi ya usiku. Basi Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni.

20 Danieli akajibu, akasema, Na lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na uweza ni wake.
Dan 2
Sasa angalia uone jambo hapa; pamoja na kwamba wakina Daniel walikua vizuri kwenye hekima na utambuzi wa ndoto lakini walisubiri kwanza Mungu awafunulie maana ya iyo siri. Uwezo waliokuwa wamepewa haukutosha kufanya kazi bila Mungu. Ule uwezo waliokuwa wamepewa kama ungekua unaweza kufanya kazi bila Mungu wasingesubiri hadi usiku wafunuliwe ndipo watoe maana ya ile ndoto. Mungu akikupa kitu anakupa si kitumike bila yeye ila kitumike kwa kumtegemea yeye zaidi.

Basi Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni.” Vs 19
Mungu akiweka kitu/ uwezo ndani ya mtu moja ya lengo lake ni kwamba asiache kuhimidiwa. Kama Danieli angejua amelitenda hilo kwa nguvu na uwezo wake kisingemsumbua kumuhimidi Mungu.
Sasa usije kuota mapembe ukiona Mungu kakupa uwezo Fulani wengine hawana ukafikiri unaweza kufanya bila yeye. Akikupa kitu uwe na uwakika kuna wakati atakuwa na matumizi na hicho kitu.

Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima 1:17

Usije kufikiri aina ya chakula waliokula kina Danieli ndiyo iliyowapa ufahamu, ni Mungu aliyewapa. Kuna wakati mwingine tunajisahau sana na kufikiri labla ivi tulivyo ni kwa sababu ya kitu fulani na kusahau uwezo wa Mungu. Kufanya hivyo ni kutokujua Mungu katika upana wake.
Biblia inamtambulisha Mungu kwetu kama “YEHOVA JIRE” ikiwa na maana ni Mungu atoaye “God will provide” Mwa 22:14
Kama Mungu alimpa Abraham kondoo from nowhere, He is God who provide knowledge to Daniel from nowhere.
Billy Brice said to Edwin one day:

 “Edwin, if Christians would only give over and above their reasonable service, the Lord would give over and above the usual blessing.”

Daniel and his friends understood this principle, and God blessed them for acting on it

Mungu alishangwazwa na uamuzi wa kina Danieli wa kutojinajisi naye akona awashangaze kwa kuwapa hekima. Tafuta cha kumshangaza Bwana ili naye akushangaze

TAFAKARI YAKO
Theme images by centauria. Powered by Blogger.