YESU NI MZABIBU-SEHEMU YA PILI
JAMBO
LA TATU
Yesu
ni mzabibu nasi tu matawi
Isaya 5
7 Kwa maana shamba la
mizabibu la Bwana wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda
ni mche wake wa kupendeza; akatumaini
kuona hukumu ya haki, na kumbe! Aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na
kumbe! Alisikia kilio.
Nataka uone hili neno
“Yuda ni mche wake” kisha linganisha
na neno “mimi ni mzabibu”. Kumbuka
Isaya anasema “Nyumba ya Israel”
ndio shamba la Bwana. Maana yake kutokea kwenye shamba linaitwa nyumba ya
Israel amempanda Yuda kama mche/mzabibu/mzabibu ulio mzuri.
Sasa rejea mfano
wa shamba la mizabibu na mzabibu mwitu uliozaliwa. Mungu alipoingia gharama ya
kumtafuta Daudi alitegemea nyumba ya Yuda (mche) ungetoa zabibu njema matokeo
yake ukatoa zabibu mwitu. Mungu alitumai kuona hukumu ya haki kumbe aliona
dhuluma (zabibu mwitu), alitumaini kuona haki na kumbe kilio. Kwa
ivyo moja ya matunda unapaswa kuzaa ukiwa ndani ya Yesu ni haki. Sasa ni kazi ndogo jitathimini inapofika kusimamia haki unakua upande gani?
Yer 23
5 Tazama siku zinakuja,
asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi
Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya
hukumu na haki katika nchi.
Isaya
11
1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
Sababu ya Yesu kujiita
mzabibu ilitokana na kwamba yeye ni chipukizi.
Chipukizi sio mti halisi isipokua ni mti ulio chomoka kwenye mti uliokuwepo
ukalala bila kuota. Kwenye nyumba ya Yuda kuna kitu Mungu alikua
akikigharamikia kikampa matokeo asiyo tarajia. Kwa ivyo ilibidi amuandae mtu
toka kwenye nyumba ya Yuda. Sasa kama yeye ni chipukizi ndio sababu anajiita
mzabibu huku akijua kuna mwenye shamba la mizabibu na ana matarajio na ilo
shamba kuzaa kitu.
Mzabibu
na Matawi
Ayu 14
8 Ijapokuwa mizizi
yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo;
9 Lakini kwa harufu ya
maji utachipuka, Na kutoa matawi kama
mche
Mzabibu ulitegemewa kutoa matawi (mimi na wewe) yanayosemwa
hapa ndiyo yale kwenye Yohana 15
JAMBO
LA NNE
Idadi
ya vilivyo zaliwa
Yoh 15
2 Kila tawi ndani yangu
lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.
“Kila
tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa” kama Yesu angekuwa ni yeye mwenye kuondoa
ilo tawi lisilo zaa angesema “naliondoa”. Kusema huliondoa maana yake hiyo sio
kazi yake ni kazi ya mwenye shamba. Maana yake ni kwamba mkulima yuko kifaida
kuliko tunavyoweza kuzani. Yeye hakimsumbui kuwa ndani ya Yesu kinachompa shida
ni kuwa ndani ya Yesu bila kuwa na faida. Kwa ivyo hana huruma kusema akuache
kwa kuwa uko ndani ya Yesu, atakuondoa tu.
Nataka uelewe
kwamba kuna watu wako ndani ya kanisa na niwazuri sana ndani ya Yesu lakini
hawana faida yoyote ile. Mbingu utaiona ila utatembea chini ya kiwango ukiwa hapa duniani.
Mfano wa Kabaila
Luka 19
2 Basi
akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie
ufalme na kurudi.
13
Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha,
akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.
15 Ikawa
aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha,
ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
16 Akaja
wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
17
Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno
lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
20 Akaja
mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika
leso.
21 Kwa
maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
22
Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa
chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka,
na kuvuna nisichopanda;
26
Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa,
bali yule asiye na kitu atanyang'anywa hata alicho nacho.
Huu mfano wa kabaila Yesu
anataka tujue umuhimu wa kumzalia matunda/ kumtengenezea faida. Huyu mjakazi
mpumbavu huenda akawa anawakilisha wakristo wengi sana ambao ni mahodari wa
kushiriki ratiba zote za kanisa lakini sio wazalishaji wa chochote katika kumtengenezea
Yesu faida. Jiulize una watu gani unajivunia kuwa ulimzalia Yesu tangu akupe
neema uokoke?
Itaendelea.....
Itaendelea.....