Header Ads

UMILIKI KATIKA UFALME

Shalom
Leo tujifunze kidogo kuhusu umiliki katika ufalme. Hii inalenga namna ambavyo Mungu anamiliki vitu na shetani anavyomiliki. Katika kuelewa tuangalie angalu kwa ufupi, namna Yesu alivyoulizwa na mafarisayo kuhusiana na dinari, baada ya kumpamba kwa maneno mazuri.
Wakasema;
“Tuambie basi, Wewe unaonaje? Ni halali kulipa kodi kwa Kaisari au la?’’ Lakini Yesu akijua makusudi yao mabaya akawaambia, ” Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega ? Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi. ” Wakamletea dinari. Naye akawauliza, ”Sura hii na maandishi haya ni vya nani ?” Wakamjibu, ‘‘Ni vya Kaisari.’’ Basi Yesu akawaambia, ‘‘Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.’’ (Mathayo 22:17-20)
 Mafarisayo walimtega kwa Swali hili ili wapate sababu ya kumsitaki, kama akisema sio halali. Lakini Yesu hakajibu ndio au hapana akaamua awaambie namna mambo ya ufalme na jinsi inavyostahili. Yesu alipodai ile Sarufu akawauliza hii sarafu ina chapa au sura ya nani? Wao wakajibu ina chapa ya CHAPA /SURA ya Kaisari. Jibu la Yesu baada ya hayo ndilo la muhimu sana na ndicho tunajifunza.  Yesu akawaambia “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu”.
Sentensi hii inajengwa kwamba yeye aliye na chapa katika kitu ndiye mmiliki na anakistahiri hicho kitu. Inawezekana mafalisayo hawakumwelewa kwa sababu ilikuwa sentensi ya kifalme. Mtu anapotaka kumiliki kitu chake kihalali, anaweka mhuri au chapa yake na mtu mwingine hawezi kuchukua.
Yesu anawaambia kama dinari hii ina chapa ya kaisari, Kaisari anaistahiri kwa sababu ni milki na muda wowote anaweza kuihitaji (Claim), lakini ingekuwa na chapa ya Mungu, haisari angepoteza uhalali na kwa sababu hiyo angepewa Mungu.
Ona, Shetani anapotaka kutawala na kukimiliki kitu anakiwekea chapa yake, kuonesha kwamba anaweza kuhitaji na kukitumia muda wowote. Na Mungu hivyo hivyo. Kabla ya kuokoka kwa mtu, Shetani anakuwa na chapa yake, kwa hiyo atamtumia muda wowote anaomhitaji (He can claim that person any time). Lakini anapookoka, damu ya Yesu inatangua ile chapa (umilki) ya shetani na kuweka chapa yake.
“Ninyi pia mliingia ndani ya Kristo mliposikia Neno la kweli, Injili ya wokovu wenu. Mkiisha kuamini, ndani yake mlitiwa MHURI, kwa yule Roho Mtakatifu wa ahadi mliyeahidiwa, yeye ndiye amana ya urithi wetu hadi ukombozi wa milki yake kuwa sifa ya utukufu Wake”. Efeso 1:13-14
 Mhuri unaonesha upande gani tupo na nani anatumiliki (the seal shows where we belong and who own us). Shetani hawezi kukudai, kwa sababu akumiliki tena. Lakini BWANA anatumiliki na anauhuru wa kutufanyia chochote anachotaka. Kama unatamani kumiliki vitu, kanuni nyepesi unafuta mhuri ambao Shetani aliuweka kwa damu ya Yesu, na kupiga mhuri wa Roho mtakatifu. 
Kama shetani ameweka mhuri katika sehemu fulani ya maisha yako, na unashindwa kutoka hapo, utangue huo mhuri kwa damu ya Yesu na weke mhuri wa Roho mtakatifu. Alafu mwambie, Mungu ndiye animilikie wala sio wewe. (God own me and I belong to Him). 

 
Theme images by centauria. Powered by Blogger.