SHUKRANI
Mhubiri
3:4 “Kuna wakati wa kulia na wakati wa
kucheka”
Kunaweza
kuwa na tafasili nyingi kadri Roho wa Mungu anavyoweza kuweka kiu ndani ya moyo
wa mtumishi wake. Leo tutazame hili andiko juu ya hizi nyakati mbili “kulia” na
“kucheka” kwa maana ya kukosa kile ulichokusudia kukipata. Mtu anaweza kweli
kulia kwa kukosa kile alichokusudia kukipata ila aliye ndani ya Kristo
hatutarajii kukuta ana wakati wa kulia juu ya kile alichokikusudia na hakakosa.
Wakati wa kulia upo kwa mtu aliye nje ya Kristo Fil 4:4, 1Thes 5:16 “Furahini siku zote”
Wakati wa kucheka
Huu
wakati wa kucheka twende na maana kwamba wakati ambao mambo yako yanakwendea
vizuri. Sasa agano jipya linachokitaka ni kwamba yameenda vizuri au vibaya ile
tu kwamba uko ndani ya Kristo furahi.
Sasa
angalia hapa: -
1Thes
5:18 “Shukuruni kwa kila jambo maana hayo
ni mapenzi ya Mungu kwenu”. Ukisoma kwa tafasili ya kiswahili ninachotaka
ukione hutokiona. Let read it in Holy Bible (ESV) “give thanks in all circumstances for this is the will of God in Christ
Jesus for you”
“in all circumstances”
Nilitaka
uone ilo neno. Kwa tafasiri isiyo rasmi ya kiswahili ni “ukiwa ndani ya hali zote”.
Maana
yake ni kwamba incase uko ndani ya majanga tayari au uko ndani ya hasara yani biashara
haijaenda sawa hapo ndipo pa kushukuru Mungu maana kama ulikua ndani ya Kristo
hayo ni mapenzi yake kwako. Sasa huwezi kufanya iyo shukrani kama kuna wakati
unalia. Hii ili kuiweza kuifanya lazima ufurahi siku zote. Kulia wakati
ulilolikusudia hujalipata ni kujiandaa tu kulalamika na sio kushukuru.
Ninaelewa ukowakati unaweza kulia kwa lengo la kuondoa uchungu ulio nao bila
kulalamika.
Jaribu
kufikiri una mwanamke kisha gafla baada ya kufanya hatua zote ili umuoe
linatokea jambo la kuwatenganisha. Kama uko ndani ya Kristo yakupasa tu ufurahi
kisha umshukuru Mungu. Nasema ivi kwa
sababu huenda kuachana na huyo mwanamke ni Mungu kakuepusha kufuatana na Mhubir
7:26
“Nami nimeona lililo
na uchungu kupita mauti, yaani mwanamke ambaye moyo wake ni mitego na tanzi, na
mikono yake kama vifungo; yeye ampendezaye Mungu atamponyoka bali mwenye dhambi
atanaswa nay eye”.
Maana ikiwa ataacha uoe hapo ndio kusema
umejichomoa jumla ndani ya mapenzi yake.
Lengo:-
Nimesema
haya yote ili tunapo mshukuru Mungu kwa yote tuliyokuwa nayo ndani ya mwaka huu
tumshukuru kwa uhalisia kabisa. Huenda kuna vitu ulikusudia vitokee mwaka huu
vijatokea mshukuru Mungu. Huenda iyo kazi uliyo ndani yake sasa si ile
uliikusudia mshukuru Mungu hata ukiwa ndani ya ilo usilolipenda ni mapenzi yake
kwako uliye ndani ya Yesu.
Ukiona
unataka kuomba then kushukuru kunajaza moyo wako dont rush just concentrate on
that kushukuru kuna breakthrough kama hujui. Wana wa israel siku moja walifanya
maandalizi ya kuimba na kusifu ila kabla ya kuanza walijikuta wakisema
Mshukuruni Mungu kwa maana fadhili zake ni za milele. Those words invited
breakthough to go before them, 2Nyak 20:21
Mshukuru
Mungu unamaliza mwaka na kujiandaa kuingia mwaka mwingine.